SAMATTA AISAIDIA KRC GENK KUINGIA ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE.

Samatta
Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta aliisaidia timu yake kuingia robo fainali ya michuano ya UEFA Europa League dhidi ya KAA Gent licha ya mchezo huo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Samatta alipachika mabao mawili katika mchezo wa awali na hivyo KRC Genk kusonga mbele kwa jumla ya mabao 6-3.

MATOKEO MENGINE
Besitkas imeingia robo fainali kwa jumla ya mabao 5-2 dhidi ya Olympiakos, Celta Vigo ilishinda 4-1 dhidi ya FK Krasnodar, Ajax imeishinda FC Copenhagen kwa 3-2, FC Schlake imesonga mbele kwa magoli ya ugenini dhidi ya Borussia Monchengladbach katika mechi mbili zilizomalizika kwa 3-3. Roma ya Italia iliweza kuingia robo fainali kwa kuichapa Lyon kwa jumla ya magoli 5-4 na Anderlecht kusonga mbele kwa 2-0 dhodo ya Apoel Nicosia.


Droo ya Klabu Bingwa Ulaya na Europa League itafanyika Ijumaa Machi 17.

0 comments: